VHM

Pages

Wednesday, April 23, 2014

NGUVU NYUMA YA JINA LAKO na Mchungaji Peter Mitimingi.

Picha: BAADHI YA WATU WALIOBADILISHWA MAJINA KATIKA BIBILIA:
THE POWER BEHIND YOUR NAME
Vitabu vinapatikana sasa 5000Tsh

1. Abramu – Ibrahamu – Alibadilishwa na Mungu Mwenyewe
• Tafsiri ya jina Abramu ilikuwa ni MUUMBAJI WA NAFSI (a souls creator; High father), maana ambayo Ilikuwa na uhusiano na mambo ya kishirikina. Ni kama wale wataalam wa kiganga. Alibadilishwa  kwenda Ibrahimu – Baba wa mataifa.
2. SARAI –SARA- Alibadilishwa na Mungu Mwenyewe
• Jina Sarai - lilimaanisha Binti wa kifalme. Tatizo lilikuwa ni binti wa Kifalme, katika ufalme upi. Ndiyo maana Mungu akaamua kufanya badiliko dogo katiaka jina lake.
• Jina Sara - linamaanisha Mwanamke aliye katika ngazi ya juu, mama wa mataifa mengi.
• Mungu alimbadilisha Sarai jina ili kuonesha hatua ya badiliko kutoka katika hatua ya chini kwenda hatua ya juu na kumfanya kuwa mama wa mataifa. (The name-change indicates a step from local to global)
3. Yakobo - Israeli - Alibadilishwa na Mungu mwenyewe.
 
• Jina Yakobo/James – lilimaanisha mtu mdanganyifu, mwenye hila
• Jina Israeli -  linamaanisha taifa la Mungu.
4. Simoni mwana wa Yohana – Petro– Alibadilishwa na Yesu.
• Jina Simoni – lilimaanisha ………………………….
Jina Petro – lilimaanisha jiwe/ mwamba

5. Sauli – Paulo – Alibadilishwa na Yesu
• Sauli ilimaanisha mtu wa maangamizi/kifo (Angalia Sauli wa Agano la Kale alitafuta kumuangamiza Daudi. Aliangamiza watu wengi sana katika utawala wake. Sauli wa Agano Jipya naye alitafuta na kuangamiza wakristo wengi sana mpaka pale alipookolewa.

• Paulo ilimaanisha mtu mdogo aliyejishusha.

6. Daniel  - Belteshaza - Alibadlishwa na mkuu wa matowashi wa mfamle Nebukadreza 
danieli na wenzake walipofika tu uhamishoni, kitu cha kwanza kilikuwa ni kubadilishwa majina yao.
Jina Danieli – lilimaanisha mtumwa w…..
Watu wengine waliobadilishwa majina yao kwenye maandiko utajisomea mwenyewe kwenye kitabu hiki NGUVU NYUMA YA JINA LAKO
BAADHI YA WATU WALIOBADILISHWA MAJINA KATIKA BIBILIA:
THE POWER BEHIND YOUR NAME
Vitabu vinapatikana sasa 5000 Tsh.
 
Kitabu hiki sio cha kukosa. haya ni baadhi tu ya majina na maana zake. Wasiliana na Mchungaji Peter Mitimingi kwa namba 
0713 183939 ili akuelekeza mahali pa kukipata kitabu hiki.
Haya ni baadhi tu ya majina na maana zake kwa ufupi.
 
1. Abramu – Ibrahamu – Alibadilishwa na Mungu Mwenyewe
• Tafsiri ya jina Abramu ilikuwa ni MUUMBAJI WA NAFSI (a souls creator; High father), maana ambayo Ilikuwa na uhusiano na mambo ya kishirikina. Ni kama wale wataalam wa kiganga. Alibadilishwa kwenda Ibrahimu – Baba wa mataifa.
2. SARAI –SARA- Alibadilishwa na Mungu Mwenyewe
• Jina Sarai - lilimaanisha Binti wa kifalme. Tatizo lilikuwa ni binti wa Kifalme, katika ufalme upi. Ndiyo maana Mungu akaamua kufanya badiliko dogo katiaka jina lake.
• Jina Sara - linamaanisha Mwanamke aliye katika ngazi ya juu, mama wa mataifa mengi.
• Mungu alimbadilisha Sarai jina ili kuonesha hatua ya badiliko kutoka katika hatua ya chini kwenda hatua ya juu na kumfanya kuwa mama wa mataifa. (The name-change indicates a step from local to global)
3. Yakobo - Israeli - Alibadilishwa na Mungu mwenyewe.

• Jina Yakobo/James – lilimaanisha mtu mdanganyifu, mwenye hila
• Jina Israeli - linamaanisha taifa la Mungu.
4. Simoni mwana wa Yohana – Petro– Alibadilishwa na Yesu.
• Jina Simoni – lilimaanisha ………………………….
Jina Petro – lilimaanisha jiwe/ mwamba

5. Sauli – Paulo – Alibadilishwa na Yesu
• Sauli ilimaanisha mtu wa maangamizi/kifo (Angalia Sauli wa Agano la Kale alitafuta kumuangamiza Daudi. Aliangamiza watu wengi sana katika utawala wake. Sauli wa Agano Jipya naye alitafuta na kuangamiza wakristo wengi sana mpaka pale alipookolewa.

• Paulo ilimaanisha mtu mdogo aliyejishusha.

6. Daniel - Belteshaza - Alibadlishwa na mkuu wa matowashi wa
mfamle Nebukadreza
danieli na wenzake walipofika tu uhamishoni, kitu cha kwanza kilikuwa ni kubadilishwa majina yao.

Jina Danieli – lilimaanisha mtumwa w…..

Watu wengine waliobadilishwa majina yao kwenye maandiko utajisomea mwenyewe kwenye kitabu hiki NGUVU NYUMA YA JINA LAKO
 

12. Agness Asili ya Kiyunani, na maana yake ni “ safi, takatifu”.
13. Adamson – Asili ya Kiingereza ya zamani, na maana yake ni “mwana wa Adamu”.
14. Aden- Asili ya Kigiliki, na maana yake ni “moto”.
15. Aisha – Asili ya Kiarabu, na maana yake ni “ yu hai na mwenye afya njema”.
16. Aaliya – Asili ya Kiarabu, na maana yake ni “mwenye asili ya kifahari”.
17. Amina – Asili ya Kiarabu, na maana yake ni “aliyemkweli na mwaminifu”.
18. Anisa – Asili ya Kiebrania, na maana yake ni “neema au upendeleo/kibali”.
19. Michael – ni nani aliye kama Mungu.
20. Amani – Asili ya Kiarabu, na maana yake ni “ hamu; matarajio au matakwa”.
21. Samson – Asili ya Kiebrania, na maana yake ni “Jua”.
22. Nicholas – Asili ya Kiyunani, na maana yake ni “watu wa ushindi”.
23. Margaret – Asili ya Kiyunani, na maana yake ni “Lulu mwanamke wa thamani”.
24. Ester – Asili ya Kiajemi, na maana yake ni “Mtu mwororo, jani la mti mwororo,”.
25. Faraja – Asili ya Kiswahili, na maana yake ni “faraja, nafuu au pumziko”.
26. Editha, Edith – Asili ya Kiingereza, na maana yake ni “Mwanamke wa mashindano kwa ajili ya mali”.
27. Jane – Asili ya Kiebrania, na maana yake ni “neema ya Mungu”.
28. Halima – Asili ya Kiarabu, na maana yake ni “mpole, mwenye tabia ya kati.”
29. Linda – Asili ya Kihispania, na maana yake ni “mzuri wa sura”.
30. Flora – Asili ya Kilatini, na maana yake ni “Ua”.
31. Victoria/Victor - Asili ya Kilatini, na maana yake ni “ushindi”.
32. Jessica – Asili ya Kiebrania, na maana yake ni “Anayeona”.


33. Emma – Asili ya Kifaransa na Kijerumani ya zamani, na maana yake ni “yote, ya kiulimwengu

VHM WAVAMIWA NA KUIBIWA WAKIWA NJIANI KUELEKEA KWENYE HUDUMA MKOANI MOROGORO



Kundi la wainjilisti ama makomandoo wa Yesu kutoka huduma ya sauti ya matumaini au The Voice of Hope ministries iliyochini ya mchungaji Peter Mitimingi, wamevamiwa na watu wasiojulikana na kuporwa pesa zote walizokuwa nazo pamoja na vifaa vingine vya kazi wakati kundi hilo likiwa njiani kuelekea Matombo mkoani Morogoro kwaajili ya huduma.

Ambapo kwa mujibu wa mchungaji Mitimingi anasema pesa zilizoporwa pamoja zilikuwa zimehifadhiwa na mweka hazina wa safari hiyo ambaye alijeruhiwa kwa kupasuka kidogo kichwani baada ya kupigwa na chupa ya bia wakati alipojaribu kuleta ubishi wa kutoa pesa kwa watu hao. Kwa mujibu wa mchungaji Mitimingi anasema timu imekwama kuendelea na safari 'tunasubiria neema ye Bwana waendelee na safari ya huko Matombo' amesema mchungaji Mitimingi.

Kuwasiliana na timu ya VHM piga namba hii kwa maswali au kuchangia huduma yao ambayo imefanyika baraka kwa maelfu nchini kwasasa. kwa walionje ya Tanzania anza na +255 713183939 na kwa walio Tanzania piga 0713 183939.

Saturday, April 12, 2014

MADHARA YA WAZAZI NA NDUGU KUMCHAGULIA MTU MUME AU MKE WA KUOLEWA NAYE


 Na Mchungaji Peter Mitimingi


1. Kuchaguliwa mwenza na wazazi. Familia nyingi za Kiafrika huwa zinavunjika kwa sababu hii.

2. Imekuwa ni kawaida hasa kwetu Waafrika kwa sababu ya urafiki wa kifamilia wazazi wa familia hizi mbili wanaweza kuamua na kuchagua wenza wa watoto wao kwa lengo la kuendeleza na kudumisha mahusiano yao kwa kupitia ndoa ya watoto wao.

3. Kuoa au Kuolewa kwa Kuwafurahisha Wanandugu. Kuoa au kuolewa kwa nia ya kutimiza matakwa ya ndugu na wanafamilia wako vilevile ni moja ya sababu zisizo sahihi za mtu kuoa au kuolewa. Ndoa sio ya ukoo ndoa ni ya watu wawili nan i lazima wakubaliane wao wenyewe bila ushawishi wa mtu wa tatu.

4. Kama ilivyo kuoa au kuolewa kunako waumiza wazazi wako, haipaswi mzazi kwa akili zake timamu amlazimishe kwa manufaa yao wenyewe binafsi, kwani itakuwa ni kumuumiza mtoto wake.

5. Hakuna mtoto ambaye kwa kufikiri kwake sawa sawa atafunga ndoa kwa minajili ya kuwaumiza wazazi wake au kuwakera. Ndoa kwa hali hiyo itakuja na changamoto zake na mambo yake, mambo mengine yanaweza kuwa ni magumu sana kuyakabili katika ndoa.

5. Kila mmoja kwa sehemu yake yaani wanaotarajia kuoana au kwa upande wa wazazi, nimuhimu kufuata taratibu zinazohusika ambazo hazitaweza kuumiza upande wowote. Let it be win-win situation. Wazazi washinde na watoto washinde pia.